Jeneza la mawe ni aina fulani ya mtungi inayotumika kuweka au kuhifadhia mfu au maiti. Halo mwanzo, Mungu alimuumba mwanadamu katika mfano wake mwenyewe na kuwapa Adamu na Awa tabia iloyowafaa. Lakini wanadamu wakaamua kuchukua njia nyingine ambayo ni tofauti na ile walopewa na Mungu mpaji wa uhai.Hayo yote yakawa ukweli mchungu wakati mwanadamu alifuata usawa usio wa kweli kati ya kiumbe na muumbaji. tangu hapo sasa, mfano halisi wa mwanadamu unaowakilisha chapa ya Mungu uliweza kufungiwa katika jeneza la mass. Jeneza hili halina Haki ya kuulinda uhalisia wangu bali kuuficha na kunipa uhalisia wa uongo ambao ni wa matrix. jeneza hili linalofunika picha yangu halisi huwakilisha Mimi mwenyewe na Hii tabia mpya niloazima ambayo ni nakala ya uongo inawakilisha roho ya uasi na maringo.
Kwa bahati mbaya, Mimi kama mwanadamu nimezoea sana jeneza langu la mawe la Matrix hadi siwezi kunusa au kugundua mabadiliko ninayopitia. kutoka kwa mwana wa mfalme hadi mtumwa wa matrix na kwa sasa Mimi kama mwanadamu nimekuwa mmoja na matrix kwa kuikataa tabia nilopewa na Mungu kule Edeni. kwa mfano mhuri wa Mungu kwangu umefungiwa katika jeneza hili la mawe. Ni lini ntafungua macho na kuona kuwa huyo mfalme wa giza amenifunga kwa jeneza la mawe la kiroho? na pia kunifanya nikamwamini? Ni lini ntagundua kuwa hadi niikane nafsi yangu inayonuka uasi siwezi nikatoka katika jela hili la kiroho la matrix. Ni lini ntaamua kuhama Matrix na kuifanya hali yangu halisi kuwa kama ya Yesu hali nilitopatiwa katika shamba la Edeni . Wakati umefika wa kutoka nje ya hili jeneza langu la mawe.